Posts

MAISHA YA CHUONI, TAMATI NIMEFIKA

 Kumbukizi za kujiunga na Chuo Kikuu cha Kiufundi cha Mombasa almaarufu Technical University of Mombasa,bado zimo akilini mwangu.Siku hiyo ya kujiunga na Chuo hiki ilikuwa Jumatatu ya tarehe ishirini na tano ya mwezi Januari mwaka wa elfu mbili ishirini na moja masaa ya asubuhi.Hapo awali nilikuwa nimepata mwaliko wa kujiunga na Chuo hiki kusomea taaluma ya habari na Mawasiliano.Ni ndoto ambayo nilitamani Sana siku moja kuwa mwanahabri tajika kama Rashid Abdhalah wa runinga ya Citizen.Siku hiyo nilivalia suti ya rangi nyeusi tititi na shati leupe pepepe kama maziwa huku likiwa limepigwa pasi kiasi ya kwamba nzi angetua juu ya shati hilo basi angefariki papo hapo. Nilifika katika afisi za usajili wa wawanagenzi,nikakabidhiwa barua ya usajili kisha nikaamuriwa kujaza nafasi zilizoachwa wazi.Kwa kuwa ilikuwa siku yangu ya kwanza kukanyaga chuo hicho,sikuwa na budi ila kuomba msaada wa kuelekezwa jinsi ya kujaza fomu hiyo.Kulitokea janadume ila lilinipea masharti ambayo sikuweza kuyaep...
Image
  MACHO YOTE SASA YAELEKEZWA KWA VIJANA KATIKA KUFUFUA UCHUMI WA TAIFA                 Picha angavu kwa hisani ya Google Je, vijana wana umuhimu wowote katika kufufua uchumi wa Kenya? Hilo ndilo swali ambalo linazidi kuumiza mishipa vichwani mwa waja wengi katika siku za hivi sasa.Hali ya uchumi imeenda juu kiasi kwamba imekuwa donda sugu lisilopona.Mamia ya waja wanazidi kupoteza maisha yao kila uchao kutokana na njaa ambayo imesababishwa na gharama ya juu ya maisha.Familia nyingi haziwezi kujimudu tena sikwambii kutosheleza mahitaji yao ya kimsingi.Habari zinazongonga vichwa vya wanahabari kila uchao ni kwamba suluhu itapatikana wapi ili kuokoa maisha ya binadamu?Wanahabari kote nchini wapo ange kuhakikisha kuwa wanataoa taarifa kemkem kuhusu familia zilizoathirika kutokana na kupanda kwa uchumi hapa nchini.Ni lazima kama ibada kuwa kilicho na sifa acha kipewe sifa, hii ni kumaanisha kuwa hongera kwa wanahabari wetu waliosimama kidete na ...

MABADILIKO YA HALI YA ANGA, MAJONZI KWA BINADAMU

 Labda nikisema dalili za kiama zimeanza kuonekana nitazidi kuumiza mitima ya waja hapa duniani, ila kusema ukweli ni kwamba watu wanazidi kuumia na kuteseka kila uchao kutokana na mabadiliko ya ghafla ya hali ya anga.Ni mara ngapi tumesikia vifo vya watu kutokana na makali ya njaa ambayo yamechangiwa na tabianchi? Hapo awali enzi za babu za babu zetu mambo yalikuwa nywee! Yani asili hizo maisha yalikuwa matamu kama asali sikwambii halua, watu wa jadi hizo waliishi maisha ya raha na starehe huku wasijue bei ya vyakula ni nini.Maisha yao yalikuwa shwari kama ya peponi ila sasa,ni vilio na simanzi kila pembe ya taifa letu tukufu la Kenya. Walumbi husema,msiba wa kujitakia hauna kilio lakini huu wa sasa uko na kilio kikubwa sana.Kila jambo mtu analonuia kulifanya ni lazima kama ibada kukadiria matokeo yake yatakuwaje kabla kuamua kulifanya.Shida nyingi tunazopitia tumezichangia sisi wenyewe,tumekumbatia kikiki mfumo mpya wa kitekinolojia ambao umetuathiri sisi binafsi vibaya. Jambo la...

BAADA YA DHIKI FARAJA

 Babu yangu,Mzee Abdhalah angefufuka leo kisha aone vile halaiki ya watu wanavyoumia kutokana na gharama ya juu ya maisha, angeanguka na kuzimia.Atakapozinduka angemwomba Maulana amrudishe katika kaburi lake huko Kilifi au angekubali mwenyewe kuendelea kuishi ili ajionee masaibu yanayowakumba wajukuu wake kutokana na garama ya uchumi. Baada ya wakazi wa Kaunti ya Mombasa kuteseka kwa miaka na mikaka kufuatia kuhamishwa kwa  huduma za mamlaka ya bandari  Nchini Kenya na kupelekwa Kaunti ya Naivasha,sasa ni afueni kwao kwani hatimaye baada ya kuapishwa kwa Rais wa taifa William Samoei Ruto,aliamuru mara moja kurejeshwa kwa huduma za bandari mjini Mombasa.  Je,kuna manufaa yoyote kwa wakazi wa Kaunti ya Mombasa kwa kurudishwa kwa huduma za bandari? Wahedi,ni tabasamu sasa kwa wakazi wote wa pwani kwani nafasi za ajira zitajaa pomoni huku waliokosa vibarua kwa muda mwingi watapata nafasi nzuri ya kufanya kazi bandarini.Fauka ya hayo,idadi ya vijana ambao wamejiingiza kwe...

HALUWA SI TAMU TENA VYUONI

Ukishikwa shikamana Nakubaliana na wasanii asilimia mia kwa mia walipoimba kuwa mapenzi ya siku hizi ni ''COME WE STAY'.Mapenzi ya siku hizi yamegeuka na vilio kila pembe ya dunia.Vile vile kumpenda mtu italingana na moyo wako,je umeridhia kueka mtu kwa nafsi au la? Kuna wengi wamewahi kuwa kwa mapenzi na mwishowe kufurahia wengine kuumia mitimani mwao kiasi cha wengine kujitoa uhai.Unaweza kupenda au kupendwa na baadae ukatendwa huku ukiishia kujutia maishani,unabaki kusema tu 'laiti ningalijua'. Mapenzi ni nini?Mapenzi ni idadi kadhaa ya hisia za ndani ,zisizoelezeka ,za kudumu kwa mtu mwingine,kuanzia mahaba ,pendo hadi upendo wa Kimungu. Kulingana na mada ya 'Haluwa si tamu tena vyuoni' ina maana kuwa mapenzi ya vyuoni yamechangia mambo mengi sana,mazuri na mabaya yake na yamekuwa kikwazo kwa baadhi ya wanagenzi. Mapenzi ya vyuoni yamezidi kushamiri sana kila uchao baina ya wanafunzi.Si Jambo la kutamausha kwani wakati mwingine pia utapata walimu wanaan...

MALEZI

UDONGO UWAHI UNGALI MAJI October 1, 2022 Malezi Malezi ni hali ya maandalizi ya mtoto kutoka utotoni hadi ukubwani ili kumwezesha kukua,kukubalika na kushiriki kwenye shughuli za kijamii kwa kumlinda na kumpatia mahitaji na huduma za kimsingi. Kutokana na maana hiyo ya malezi ,basi ni sharti kama ibada ,kwa mzazi yeyote kuwa na mipango kabambe dhidi ya mtoto ili kufanikisha malezi murua. Jambo la kutamausha katika Karne hii tunayoishi ni kwamba ,asilimia kubwa ya wazazi wameyaepuka majukumu yao na  kusahau wajibu wao kwa watoto wao.Hali hii imechangiwa na mfumo wa kidijitali ambao umefanya wazazi wengi kuyaelekeza majukumu yao kwa wafanyikazi wa nyumba. Siku hizi mzazi anathamini sana vifaa vya kielektroniki mfano simu hususan muda wa mapumziko baada ya kutoka kazini kuliko kukaa chini na mwanawe na kuzungumza mawili matatu.Hali yiyi hiyi ya kutotenga muda mwafaka wa kukaa na mtoto imezidi kuwa tumbo joto kwani visa vingi vya utomvu wa nidhamu miongoni mwa watoto vimekuwa vikish...